June 06 2016 Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mark Childress alikutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli ambapo katika mazungumzo yao ameahidi kuwa Marekani itatoa dola milioni 800 kwa Tanzania kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Balozi
Childress amesema kutolewa kwa fedha hizo ni uthibitisho kuwa
kutotolewa kwa fedha za awamu ya pili ya mradi wa changamoto za milenia
(MCC-2) hakujaondoa uhusiano na ushirikiano wa Tanzania na Marekani
ikiwemo utoaji wa misaada ya maendeleo.
“Tanzania
na Marekani kupitia shirika letu la misaada la USAID tunatarajia
kutiliana saini mkataba wa zaidi ya dola milioni 400 kwa ajili ya mwaka
ujao, pia tumezungumza kuwa kutakuwa na dola milioni 800 zitakazotolewa
na Marekani kwa ajili ya miradi mbalimbali na hii haihusiani na MCC’:-Balozi Mark Childress
Kwa
upande wake Rais Magufuli amesema serikali yake itaendeleza na
kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano na Marekani na kwamba fedha za
msaada kutoka Marekani ni muhimu kwa maendeleo ya Tanzania.
‘Amekuja
kutuhakikishia kwamba watatoa hela kwa ajili ya Tanzania na anasema
sasa hivi watatoa zaidi ya dola milioni 800, na mkataba mwingine
tunaweza tukasaini hata kesho wa dola milioni 410’
‘anasema
kutotoa hela za MCC hakuna maana kupotea kwa urafiki wa Tanzania na
Marekani, urafiki wa Tanzania na marekani upo pale pale na sasa
wanaongeza hela nyingi zaidi katika kuonesha kwamba juhudi za HAPA KAZI
TU zinaendelea’:-Rais Magufuli
No comments:
Post a Comment